eti nini?
Mwanadada fulani eti kaniuliza kama najua kuandika kiswahili, kisha akapata mshangao nilipomjibu kihakika. Mwenyewe anaishi Bongo, kwao haswa ni huko Tz lakini makubwa ni kwamba yeye hajui kuandika kiswahili vile.
Haidhuru. Jambo la muhimu ni kwamba amejiunga na sarakasi ya wanablogu – hata usiku wa manane – hii sasa ninazungumza nae kwenye hotmail – hii sijui live waya, sijui live nini… saa nane usiku. Janga kubwa hili.
Nenda mcheki Sahara Soul Food umpe karibu. Na ukimuona, mwambie “kwisha yeye. kaingia pangoni hajitoi”
October 30, 2006 at 4:29 am
Wewe! Ninajua kuandika Kiswahili, ila hai-flow kama English! Halafu inanichukua forever kuandika a simple paragraph. Nimeshajaribu sana, lakini nimeona tu niwaachilie nyie wazee. Labda siku mpja nitafanikiwa.
October 30, 2006 at 5:41 am
Al Kags,
Hats off to ya’ll reppin’ propa wey in swa. Me all i can do is curse!
October 30, 2006 at 5:53 am
Heko kwako kujitoa mhanga na matumizi murwa ya lugha halisi ya taifa. Huenda utamtia moyo dada huyu ajihamasishe nae pia kujieleza vyema zaidi na kwa ufasaha unaostahili.
October 30, 2006 at 8:59 am
Nice layout!
Kiswahili and I are strange bedfellows.
October 30, 2006 at 9:00 am
@Alexcia, it will be interesting to see you learn. You write black american fairly well – I think.
@Akiey, wamuona mwanadada mwenyewe amejitokeza hapa ili kujitetea… tutamuhimiza bila shaka. Pengine una maarifa 🙂 ya kuwawezesha wengine kuzungumza?
Nawatafuta wa shairi wa kiswahili kwa kitabu changu kijayo. waelezee wengine…
Al Kags
October 30, 2006 at 3:31 pm
Mzee wa Pwani, umechapia kidogo! Naona lugha imekupiga chenga. NKN (Nacheka Kwa Nguvu). Hii inatakiwa kusema KIJAYO au KIJACHO, “… Nawatafuta wa shairi wa kiswahili kwa kitabu changu kijayo …”
October 30, 2006 at 3:39 pm
mwanadada usitie shaka. Kuteleza sio kwanguka. NKN, Mambo haya ni yale yale… ‘japokuwa naweza kujitia kwamba nimezungumza lafudhi nyngine tu… kujitetea sishindwi.
tupendane tujengane, bibiye…
Al Kags
October 30, 2006 at 3:41 pm
@ Akiey, mwanadada tumemleta nyumbani waona. Uzungu ameutupilia mbali. Vidapa amevitupa sasa anazungumza kama sisi.
Kazi nzuri, mwafrika
October 30, 2006 at 9:22 pm
kazi bora. tujikazeni kisabuni ndugu zangu, tuitetee lugha yetu. undelea na umahiri huu wa lugha …
September 9, 2010 at 10:36 pm
Waswahili hamjambo? Za kuamka… kushinda? Hongereni kwa jitihada zenu kuitukuza lugha hii tukufu ya Kiswahili. Nami nawaunga mkono.